Friday, December 30, 2016

YAMOTO BAND - NITAKUPWELEPWETA LYRICS.

[Intro]
Aaah Yamoto Band
Aa aah Yamoto!
Aaah Yamoto Band
Aa aah Yamoto!
[Verse 1]
Unajifanya bingwa wa kupenda (dada ee)
Kumbe bingwa wa kutenda kuliko kupenda(dada ee)
Tena una sifa yakuogopwa kama defender (dada ee)
Umeua wengi ila kwangu umedunda
Ah koma eh, sitaki nizikwe na kilo mbili kwenye mfuko
Mama eh, sitaki familia ilie kwa sababu yako
Dada eh, ananitegemea mama eh (a aa eh)
Nikifa atalia sana (a aah)
Katika familia na mimi ni baba japo baba yupo
Nikija kufa ufa nani ataziba ebu kwenda zako
Ananitegemea mama eh (a aa eh)
Nikifa atalia sana eh (a aa eh)
We kuku wa kizungu mchinjaji hana tabu
We kuku wa kizungu mchinjaji hana tabu
Ebu niache eh, ebu niache
Unapita na dumu la petroli ebu niache
Ebu niache eh, ebu niache
Unapita na dumu la petroli ebu niache
Una rambo, mi n’na muwa ni ujinga ujinga tu eh, mi hujaniua
Una rambo, mi n’na muwa ni ujinga ujinga tu eh, mi hujaniua
[Chorus]
Unakichaa mi nakuita we mwendawazimu
Nimepata habari mwili wako umeujaza sumu
Unang’ang’a ng’ana unataka mi kunipa utamu
Umekosa singei ngoma ya kucheza huna nenda kaicheze
Segere, segere mama
Segere segere oh
Segere segere mama
(We mwali ah nenda kalicheze)
Segere, segere mama
Segere Segere oh
Segere segere mama
[Verse 2 ]
Eti ametuma mashoga zake waje kuniambia
Roho inamuuma kidudu penzi kinamsumbua
Siri imevuma lemenyula wengi wanalipakua
Hana huruma kalitoa wapi aje kuniua
Ilikuwazia sana nikatoa nikagawanya
Nikajua unadanganya (we mbaya wee)
Nusu dengu nusu dona wengi wao unawadanganya
Mama chini we kitanda (huna haya wee)
[Bridge]
Mimi sio saizi yako nitakupwelepweta bure
Tafuta type yako wa Ilala mimi wa Kilungule
Mimi sio saizi yako nitakupwelepweta bure
Tafuta type yako wa Ilala mimi wa Kilungule
[Verse 3]
Unataka kunipeperusha we kimbunga huniwezi ng’o
Kina chako cha maji marefu kuogelea sikiwezi ng’o
Unashinda kuwinda vyenye kung’aa vya masizi huvitaki no
Unang’ang’ana kama ruba kwenye mwili wangu
We nenda zako iyee
Na ushindwe ushindwe uniache mimi mwana wa mwenzio
Kwetu ndo jembe jembe ukivunja mpini ni kilio
Na ushindwe ushindwe uniache mimi mwana wa mwenzio
Kwetu ndo jembe jembe ukivunja mpini ni kilio
[Chorus]
Unakichaa mi nakuita we mwendawazimu
Nimepata habari mwili wako umeujaza sumu
Unang’ang’a ng’ana unataka mi kunipa utamu
Umekosa singei ngoma ya kucheza huna nenda kaicheze
Segere, segere mama
Segere segere oh
Segere segere mama
(We mwali ah nenda kalicheze)
Segere, segere mama
Segere Segere oh
Segere segere mama
[Bridge]
Mimi sio saizi yako nitakupwelepweta bure
Tafuta type yako wa Ilala mimi wa Kilungule
Mimi sio saizi yako nitakupwelepweta bure
Tafuta type yako wa Ilala mimi wa Kilungule
[Outro]
Ana chuma cha moto huyoo
Anaunguza watoto huyooo
Apewe mkong’oto huyooo
Ili ifike mwisho huyooo
Tabia yake, tabia yake, tabia yake

No comments:

Post a Comment