Friday, February 10, 2017

kemosabe by Fid Q lyrics

Niliamini mapene hayatoshi..na niki-hustle siyakosi/
Sababu.. sipo kwenye loss na life simple huwa hai-cost/

Kwahivyo nikaenda Dar na treni... of thoughts../
Sikwenda kuzubaa au kushangaa nikusaka chapaa boss/

Sikutaka kuivaa mikosi..nilitaKa kuivaa mikoti/
Sikuwa na passport..password.. pin..lakini ni crack codes/

Walionisapoti wote siwaoni kwa line/
Wakini-approach ili nifungue pochi ya noti tu-shine..hatuko fine/

Je mimi ni kaka mubaya...? kaka aso haya../
KAKA..? huniitaga NAKAAYA/
Mama C huniita brother bila shaka.. Mozaya/
Niko sick & tired of being sick & tired/

Na huu ni mwaka wa ndui/ Sitaki upele urudi tena.. mnachotaka sikijui/
Nashukuru hamtopata mbawa ikiwa mtaupata huo uchui/
Mnautaka uadui? mnayempaka ni mtata.. makaka hamkui?

Mmeendekeza hila.. legeza hasira za harakati/
Mie nita-ball.... hata kwa mpira wa makaratasi/

Unaweza ukahisi mie napita tu.. kwakusahau mie nina-hustle/
Nimezaliwa Afrika.. ugumu wa maisha umenifunza ku-struggle/

Ukiwa idle.. unamu-attract shaytwan (SHETANI)/
Kichwani nina MSAHAFU na BIBLE.. life ni zaidi ya ku-have fun/

Kwani.. Kila kicheche anajiona ni mzima/
Na njia pekee ya kuepuka ngoma ni kugoma kupima/

Ikiwa maujuzi haya hayakugusi.. itanilazimu nikuelewe/
Sometimes hata kamusi.. huimiss tafsiri yenyewe/

Nalindwa na dua za mama.. tangu baba simjui/
Namfanya adui mwenye njama aache drama na akue/
Ili ajijue kabla hajakwama huko mrama asitue/
Ajikwamue kwenye lawama.. yenye maana yamchukue/

Kisha anaiombee mimi ili nifaidike kwa hizi mbio/
Siamini kwenye umasikini hivyo sihofii mafanikio/

Ndiyo.. mie ni LEO kwahiyo sifikirii kushindwa/
Zingatia kauli hiyo hausikii inaashiria ubingwa?/

Mie ni mbishi.. muulize Nikki - hatopinga/
Na hata kama ningekua mbuzi ningelala chaka la simba..

Mwana FA feat. Vanessa Mdee - Dume Suruali lyrics

Mwana FA
Hudat hudat hii ni salam na ufahamu
Kama unauza mapenzi siyo kwa binamu
Huna haja ya kusubiri hii ni hukumu
Hakuna kitu utapata utangoja kama askari wa zamu
Dume suruali dume kaptula
Shauri zako ilimradi sipati hasara
Usione utani me sihongi hata kwa ishara
Utaniambia nini mpaka unigeuze fala
Kwanza nasikia hongo zinaleta mkosi...

Sentano yangu hugusi hata ukiongea kidosi
Yabaki mapenzi tusileteane ujambazi
Hata upige sarakasi utachonga viazi.
BAHILI KAMA NINI!!!!!!!!! Ndiyo mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisikii tena
Kwani unauza nini dada!
Hunitakii mema.

Kiitikio

We dume suruali kaa mbali nami
Kama dume suruali kaa mbali nami
Huendani na mimi
I want Gucci, Fendi, spend it on the girl like me
My name is Vee Money, money spend on the girl like me

MWANA FA
Nihonge nanunua nini kwa nini yaani!
Kuna kipi nisichokijua ina TV ndani?
Usiulize n’takupa nini dada piga moyo konde
Viuno vingi kama mwali wa kimakonde
Usipende hela kama mfuko
Au fanya unavyofanya upate zako
Vishawishi vingi binti sema na moyo wako
Na ujifunze pesa zinauza utu wako
Tajiri mtata kama Salah
Zipo ila sitoi me ni balaa
Unapenda hela zangu nami nazipenda pia
Kila mtu abaki na zake bye baby tutaongea
MWANAUME WA HIVYO WA NINI SASA!!!!! Ndiyo mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisikii tena
Kwani unauza nini dada
Hunitakii mema

Vanessa
Aje aje ajeeee me mtoto fulani ghali
Nihonge gari Ma sweet sweet baby
Wanna see you today unipeleke party
Aje aje ajeee njoo nikupe TBT

MWANA FA
Siyo kwa enzi ya Magufuli
Zali ilikuwa long siku hizi hakuna la mentali
Nikikuhonga na ukiniacha nitakujia usingizini
Naepusha shari matatizo yote ya nini
Hakuna kipya chini ya jua
Hata nisiyoyafanya nishayasikia
Ningekuwa mhongaji ningeshafulia wangu
Mademu wangu wa zamani wote wangekuwa maadui zangu
MWANAUME HOVYO WEWE!!!!! Ndiyo mnavyosema
Na ukiniomba kesho hunisikii tena
Kwani unauza nini dada
Hunitakii mema

Vanessa
Baki na hamu zako

Kiitikio
We dume suruali kaa mbali nami
Kama dume suruali kaa mbali nami
Huendani na mimi
I want Gucci, Fendi, spend it on the girl like me
My name is Vee Money, money spend on the girl like me

VANESSA
Baba bure huyuu!!!

Mwana FA
Hata pantoni lina staff
Vanessa

Unamwambia nani sasa! Unamwaaambia nani sasa