Friday, December 30, 2016

Hussein Machozi Kafia Ghetto lyrsics

[Verse 1]
Siku nyingi binti namfukuzia
Alishan’tosa nishakata tamaa
Sikujua kama kwangu angekuja
Nilitoa matumaini ya kumpata
Siku nyingi binti namfukuzia
Alishan’tosa nishakata tamaa
Sikujua kama kwangu angekuja
Nilitoa matumaini ya kumpata
(Leo hii kaja mwenyewe mchumba)
Ghetto kwangu mpaka ndani kaingia
(Nilimuuliza naeza kukusaidia)
Akacheka kisha akaniambia
Ombi langu lile amenikubalia
Siku zote alikuwa akinifikiria
Niliruka kwa furaha kubwa sana
Sikuamini kama mchumba ningempata
(Usilojua ni usiku wa giza)
Ningetambua bora ningemtimua
(Usilojua ni usiku wa giza)
Ningetambua bora ningemtimua
[Chorus]
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?
[Verse 2]
Baada ya stori binti nilimuuliza
Kinywaji gani angeweza kutumia
Alinieleza kisha mi nikainuka
Nikaelekea dukani kununua
Baada ya stori binti nilimuuliza
Kinywaji gani angeweza kutumia
Alinieleza kisha mi nikainuka
Nikaelekea dukani kununua
(Huwezi amini nyuma nilipomuacha)
Baada ya kurudi ndipo kizaa zaa
(Binti alikuwa kitandani kajilaza)
Nilimuamsha lakini hakuamka
Pumzi zake zilikuwa zimekata
Nilidhani labda kazimia
Maji ya baridi kichwani nilimwagia
Lakini hata hakushtuka
(Kumbe alikuwa tayari ameshakufa)
Nimekwisha Hussein bila kujua
(Kumbe alikuwa tayari ameshakufa)
Nimekwisha Machozi bila kujua
[Chorus]
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?
[Bridge]
Ee Mola, nimekosa nini?
Ee Mola, niokoe mimi
Ee Mola basi nipe akili
Mimi nifanye nini
Ee Mola, nimekosa nini?
Ee Mola, niokoe mimi
Ee Mola basi nipe akili
Mimi nifanye nini
Furaha yangu, imekuwa kilio changu (kilio changu)
Furaha yangu, imekuwa kilio changu
Ndoto zangu leo majonzi kwangu
Ntawaeleza nini walimwengu?
Ndoto zangu leo majonzi kwangu
Ntawaeleza nini walimwengu?
(Vipi, wataniona mi ni mkweli?)
(Vipi nikiwaelezea wataniamini?)
(Vipi, wataniona sio katili?)
(Vipi, ingekuwa wewe ungefanya nini?)
[Chorus]
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?

No comments:

Post a Comment