Saturday, May 13, 2017

Ni mcheza bongo Mac Muga
Yuko single sana Mac Muga
Ukimwona kutwa kajinamia kwa sababu ya maisha yanamchanganya
Long time ago alizamia
Nakwenda kusini mwa Africa
Huku pia alitanua kwa sababu ya maisha aliyofuma
Alikuwa maarufu sana,
Akajiona yeye ndo winner
Full kujichanganya na wasichana
Club zote za huko kujulikana

Wewe Mac Muga
Wewe wewe Mac Muga
Ah, hii dunia,
Mac Muga huruma!

Chorus 2x
Mungu si Athumani alipofika South Africa alikuwa na maisha bomba
Ya juu, ya thamani tena yanayohitajika magari na kubwa nyumba x2

Ona sasa amesharejea, hajui wapi ataanzia!
Hakuna kazi kutwa kajinamia
Mac Muga hii ni dunia
Maisha alichezea, gari ya kutembelea
Shida walimwelezea wasichana na shida zao akawatatulia
Hivi upewe nini Mac Muga?
Mungu akupe nini Mac Muga?
Nyumba ulijijengea, full kutanua
Wewe ndio wewe, wengine fala!

Wewe, Mac Muga

Ona sasa umeshatibua!
South Africa wamekutimua
Na sasa home usharejea
Wewe Mac Muga
Mungu akupe nini Mac Muga?
aah hii dunia, Mac Muga huruma

Chorus 2x
Mungu si athumani alipofika South Africa alikuwa na maisha bomba
Ya juu, ya thamani tena yanayohitajika magari na kubwa nyumba x2

Ona sasa amesharejea, hajui wapi ataanzia
Hakuna kazi ila akajinamia
Mac Muga hii ni dunia!

Verse 3
Yikes kama huoni kwa Mac Muga
Huoni noma huruma kanyongonyea
Afanye nini sasa, cha kufanya
Kila anachachofanya anaona anakosea
Yikes, kama huoni kwa Mac Muga
Woi noma huruma kanyongonyea
Afanye nini sasa, cha kufanya
Kila anachachofanya anaona anakosea

Akiwa jambazi gerezani ataishia
Akiwa mwizi anaona atauliwa
Akifikiria kujiua
Nafsi inamsuta basi analia

Wewe Mac Muga!
Mungu akupe nini Mac Muga?
oo dunia Mac Muga noma
Aliy kiba wewe nakupenda daima nyimbo zako hata nisikize vipi zinabaki kuwa mpyaa kila siku leo naskiliza 2017