Friday, December 30, 2016

Chid Benz ft Alikiba --- Hasira Za NINI LYRICS

[Chorus – Alikiba]
Hasira za nini?
Kwanini huniamini
Kama mwenzio bado nakupenda?
Maneno mengi mjini, ili uniache mimi
Lakini mwenzio bado nakupenda
Hasira za nini?
Kwanini huniamini
Kama mwenzio bado nakupenda?
Maneno mengi mjini, ili uniache mimi
Lakini mwenzio bado nakupenda
[Verse 1 – Chidi Benz]
Chakula hakiliki kama nsipokuona
Haipiti chai iliki au ndafu ilionona
Laazizi, waubani, mchumba
Mashaallah, Mola kweli aliumba
Huna kasoro umejazika
Ila mlani kama godoro, kiuno umekatika
Nabangaiza vibarua mchana, usiku
Japo nipate chochote nije tule ipite siku
Maneno ya waongo wanaharibu makusudi
Usafiri mjini tabu napochelewa kurudi
Usinihisi vibaya ukanuna, ukavimba
Ukatamani unirarue, ugeuke simba
(Ugeuke simba baby, hasira za nini?
Hasira za nini, baby?)
[Chorus – Alikiba]
Hasira za nini?
Kwanini huniamini
Kama mwenzio bado nakupenda?
Maneno mengi mjini, ili uniache mimi
Lakini mwenzio bado nakupenda
Hasira za nini?
Kwanini huniamini
Kama mwenzio bado nakupenda?
Maneno mengi mjini, ili uniache mimi
Lakini mwenzio bado nakupenda
[Chorus – Alikiba]
Mami punguza hasira na unisikilize mimi
Please acha kuzira hivyo unaniumiza mimi
Sina mwingine zaidi yako haki ya nani
Moyo wangu uko kwako kwingine sitotamani
Nlizunguka pande zote, nkaona warembo wote
Kote nlisimama kwako naanguka niokote
Unanipa morali ya kutafuta mapesa
Najaza kibubu maisha mbele yasije tutesa
Pesa ndo kila kitu nazisaka mchana, usiku
Sipendi kushikwa karaha, nakwambia kila siku
Kokote kambi, chochote pwani, ndo life honey
Staki tuje lia njaa nazisaka nje, ndani
Jasho langu ili upate isikukumbe tamaa
Japo nilete mkate wakinishinda dagaa
Nipende usiniache mami, usije tambaa
Napokumbata nikumbate wangu wa shida na raha
Hasira za nini mamaa?
La Familia! Chidi Benz hapa
[Chorus – Alikiba]
Hasira za nini?
Kwanini huniamini
Kama mwenzio bado nakupenda?
Maneno mengi mjini, ili uniache mimi
Lakini mwenzio bado nakupenda
Hasira za nini?
Kwanini huniamini
Kama mwenzio bado nakupenda?
Maneno mengi mjini, ili uniache mimi
Lakini mwenzio bado nakupenda
[Outro – Chidi Benz & (Alikiba)]
Usinihukumu vibaya kwa maneno ya watu
Wabaya wasiopenda maendeleo kwa watu
(Usinihukumu vibaya kwa maneno ya watu
Wabaya wasiopenda maendeleo kwa watu)
Usinihukumu vibaya kwa maneno ya watu
Wabaya wasiopenda maendeleo kwa watu
(Usinihukumu vibaya kwa maneno ya watu
Wabaya wasiopenda maendeleo kwa watu)
Mami usinihukumu vibaya kwa maneno ya watu
Maendeleo kwa watu
Usinihukumu vibaya kwa maneno ya watu
Wabaya wasiopenda maendeleo kwa watu

No comments:

Post a Comment