Thursday, May 26, 2016

ji ft lil ghetto kidato kimoja Lyrics

[Verse 1 – JI]
Kama safari ya mapenzi, nataka kuianzisha mimi na wewe
Nimepita nimeona wengi, jua moyo umekuchagua wewe
Kama safari ya mapenzi, nataka kuianzisha mimi na wewe
Nimepita nimeona wengi, jua moyo umekuchagua wewe
Nikiwa karibu na ua ridi, basi na mimi nitanukia
Kukuoa inanibidi, kwa kila hali ma umenivutia
[Chorus – JI]
Unanikumbuka ila tu unaleta ukaidi
Mimi ni yule yule tulosoma wote kidato kimoja
Unanikumbuka ila tu unaleta ukaidi
Mimi ni yule yule tulosoma wote kidato kimoja
[Verse 2 – JI]
Unajua mtu halazimishwi kupenda, anapenda mwenyewe
Basi usinikuzishie kidonda, wakati wajua dawa ni wewe
Unajua mtu halazimishwi kupenda, anapenda mwenyewe
Basi usinikuzishie kidonda, wakati wajua dawa ni wewe
Ntapata mi au nitakosa, utanisononesha kama ukinitosa
Kiangazi hata mvua za masika, nikikukosa jua ntaweweseka
Ntapata mi au nitakosa, utanisononesha kama ukinitosa
Kiangazi hata mvua za masika, nikikukosa jua ntaweweseka
[Chorus – JI]
Unanikumbuka ila tu unaleta ukaidi
Mimi ni yule yule tulosoma wote kidato kimoja
Unanikumbuka ila tu unaleta ukaidi
Mimi ni yule yule tulosoma wote kidato kimoja
[Verse 3 – Lil Ghetto]
Naamini unanikumbuka, hizo dharau uloleta
Kama tunda limeshawiva, tulibandue maganda
Fikiri, kumbuka tulipotoka
Mama wee, dada wee, unanitesa sana
Mama wee, dada wee, mbona unanichanganya?!
[Chorus – JI]
Unanikumbuka ila tu unaleta ukaidi
Mimi ni yule yule tulosoma wote kidato kimoja
Unanikumbuka ila tu unaleta ukaidi
Mimi ni yule yule tulosoma wote kidato kimoja

No comments:

Post a Comment