Tuesday, April 3, 2018

Matatizo – Harmonize lyrics

Oi yeh Olelele Wasafi Records Alfajiri imefika Anga inang’aaa Mvua inaanza katika Ghafla tumbo la njaa Naweka sauti kwa spika Nipate umbea wa Dar Mara simu inaita Jina la Anko Twaha akisema Mama yu hoi kitandani Kama si wa leo wa kesho Na kupona sidhani Upate japo neno la mwisho Mi ndo mtoto wa pekee Nyumbani wananitegemea Mdogo wangu wa kike Hali duni alishagaolewa Tazama jasho langu la mnyonge Kipato hakikidhi mahitaji Napiga moyo konde Yarabi Mola ndo mpaji Matatizo Matatizo Yatakwisha lini Matatizo Kila siku mimi (ewe Mola) Matatizo Yatakwisha lini Japo likizo Nifurahi na mimi Mola aliniumba na subira Imani pekee ngao yangu Mbona nishasali sana Ila mambo bado tafarani Mama kanifunza kikabila Ikunde sanda haimi yangu Tena nijitume sana Na vya watu nisivitamani Hata mpenzi nilo nae Najua siku atanikimbia Itanitesa ye ndio nguzo Zile ngoja kesho Baadae atazichoka kuzivumilia Anakosa hata matunzo Ona Nadaiwa kodi nilipopanga Nashinda road nikiranda Nishapinga hodi kwa waganga Kwa kuhisi nalogwa Nikauza maji na karanga Nikawa dobi kwa viwanda Ila kote ziro ni majanga Mtindo mmoja Mi ndo mtoto wa pekee Nyumbani wananitegemea Mdogo wangu wa kike Hali duni alishagaolewa Tazama jasho langu la mnyonge Kipato hakikidhi mahitaji Napiga moyo konde Yarabi Mola ndo mpaji Matatizo Matatizo Yatakwisha lini Matatizo Kila siku mimi (ewe Mola) Matatizo Yatakwisha lini Japo likizo Nifurahi na mimi

No comments:

Post a Comment