Thursday, February 11, 2016

Nitafanya Kidum Lady Jaydee

Nitafanya

Kidum
Nitafanya by Kidum ft Lady Jaydee, Tanzania Bongo Flava Lyrics
Verse 1 (Kidum) 
Ikiwa umeamua kunitoroka 
ikiwa unahisi hujiskii nami tena 
na mbona imekuwa ngumu kunidokeza 
naona ni bora nilie leo, badala ya kesho 
kupenda, usipende 
ni kama kujitia kitanzi 
nitachimba na sururu 
kwa ardhi nikitafuta penzi lako 
ni heri nipigwe fimbo kwa mwili 
sababu ntajikuna ama ntajikanda na maji moto 
maumivu ya penzi, mtu hajikuni 
wala hajikandi na maji 
na hakuna upasuaji

Chorus 
kama 
kuna kosa nimewahi fanya (nielezee) 
kama 
kuna jinsi tunaweza leta (mpaka niishi) 
na kama 
kuna kitendo linaweza tendwa (nielezee)
nitafanya (fanya) 
nitatenda (tenda) 
nitafanya (fanya) 
nitatenda (tenda)
nitafanya (fanya) 
nitatenda (tenda) 
nitafanya (fanya) 
nitatenda (tenda)

Verse 2 (Lady Jay Dee) 
kweli hukumbuki ulioyafanya 
ni kweli unakumbuka tulikotoka 
sisemi habari zozote za kusikia 
bali kwa ushahidi niliouona 
msamaha mara ngapi 
umeshaomba na bado 
chenye makosa mangapi 
niliyoyafumbia macho 
mpaka leo nahisi kufika kikomo 
maumivu yanazidi 
ndani ya moyo 
sitaki kwenda mbali kwani uko moyoni 
nikusamehe mimi mara ngapi wee 
nielezee mpenzi mara ngapi

Chorus 
unataka nikusamehe mara ngapi (usihesabu) 
ungependa nikuvumilie mara ngapi (hii ni ya mwisho) 
je wewe nikulilie mara ngapi (vumilia)
sitoweza (utaweza wee) 
nimechoka (usichoke) 
nimeshindwa (usishindwe) 
naondoka (usiondoke)
sitoweza (utaweza yee) 
nimechoka 
nimeshindwa (usishindwe) 
naondoka (usishindwe)

Verse 3 
ukihesabu mara ngapi umenisamehe 
ni kama kuhesabu 
ni mara ngapi mtoto kaharibu nappy 
usichoke 
usiondoke 
usilie 
niko hapa kukulinda

Chorus
kama 
kuna kosa nimewahi fanya (nielezee) 
kama 
kuna jinsi tunaweza leta (mpaka niishi) 
na kama 
kuna kitendo lingeweza tendwa (nielezee)
nitafanya (fanya) 
nitatenda (tenda) 
nitafanya (fanya) 
nitatenda (tenda)
nitafanya (fanya) 
nitatenda (tenda) 
nitafanya (fanya) 
nitatenda (tenda)
unataka nikusamehe mara ngapi (usihesabu) 
ungependa nikuvumilie mara ngapi (hii ni ya mwisho) 
je wewe nikulilie mara ngapi (vumilia)
sitoweza (utaweza wee) 
nimechoka (usichoke) 
nimeshindwa (usishindwe) 
naondoka (usiondoke)
sitoweza (utaweza yee) 
nimechoka 
nimeshindwa (usishindwe) 
naondoka (usishindwe)

No comments:

Post a Comment