Monday, August 2, 2021

MwanaFA – We endelea tu lyrics

 Kwa Mungu hakuna majungu mi nina Mungu

We endelea tu (Aah aah)
We endelea tu

As you can see am ghetto and fabulous
Hella zinafanya dunia inazunguka
Let me handle this
Sihitaji beats kutingisha kichwa chako
Naflow tu kama nina beats za moyo wako

Wakikuuliza naendelea aje
Waambie vizuri zaidi ya jana
Vizuri zaidi ya wao Mungu ana manguvu sana
Miluzi mingi na kubwa la mbwa sipotei
Mipango ya miaka chungu nzima na dira hunitoi

Yeah naitika nikijisikia maisha usiyavalie kikoi
Na sio lazima yakubali kwani unayadai
Subira haivuti bangi haigongi nyagi
Inavuta heri tu na haijawahi kubugi
Kilienda kwa mganga na ka unavyoona kimerudi
Hata kama hukipendi kukiheshimu inakubidi

Mbuyu ulianza ka mchicha ila mcha haujawahi kuwa mbuyu
Sikiza walofanikiwa ongeza zako mbayu wayu
Anayejifanya anakwamua anakushika upigwe babu
Mtie mitama siku nyingine ashike adabu
Kama message sipendi boss namshoot mpaka messenger
(Boss namshoot mpaka messenger)
We endelea tu

Kwa Mungu hakuna majungu
Mi nina Mungu
We endelea tu (aah aah)
We endelea tu

Ah B Dady

No comments:

Post a Comment