Saturday, December 10, 2016

KOLABO SABA NISIZOTAMANI ZITOKEE BONGO

.ALIKIBA & DIAMOND
Hii inaweza kuwa kali kibiashara kwani inaweza kutengeneza wimbo uatakao vunja rekodi nyingi za kupakuliwa ,kutazamwa na kuleta matamasha ya ndani na nje mwanzoni.Ubora wa wimbo hautapewa kipaumbele zai namna ya kutanganzwa na kuachiwa ndicho kitakuwa kitu cha msingi sana na kuvunja Aliences ambazo zimejijenga kwa makampuni ya simu hasa kwenye kipindi cha kupiga kura za tuzo  hayatanufaika kwani kasi na ushindani wa kuwapigia kura wanamuziki hawa itapungua.
Hivyo kolabo ya wakali hawa wa muziki haitakuwa na ladha tunayotarajia kutoka kwao hivyo kwa maoni yao wasanii hawa wakitaka kufanya kolabo wasifanye peke yao aongezeke mtu wa tatu kati na kuleta uji badala ya mafuta ya taa na maji.

No comments:

Post a Comment