Friday, December 30, 2016

Hussein Machozi - Kwa ajili yako lyrics

[Verse 1]
Najua hiki ndo kipindi ukipendacho
Najua sasa hivi upo karibu na redio
Labda peke yako au na rafiki zako
Naomba kidogo ongeza sauti ya radio
Nachukua nafasi kuongea nawe kwa wimbo (uh, uu, uuh)
Nimetunga special kwa ajili yako mrembo (uh, uu, uuh)
Mtangazaji kati ya wimbo usiweke jingle (uh, uu, uuh)
Nimetunga maalum kwa mtu alie single (uh, aliye single uuh)
[Chorus]
Kwa ajili yako naimba
Sauti hii sikia
Habari hii pokea
Zingatia mrembo, usipuuze mrembo
Zingatia mrembo, usipuuze mrembo
Zingatia aah aa, zingatia ahaa
[Verse 2]
Ndani yaroho yangu uko peke yako
Usihofu mamii hakuna mwenzako
Nimezaliwa mimi kwa ajili yako
Naahidi sitotupa penzi lako
Nimekupa nafasi kubwa ndani ya moyo (uh, uu, uuh)
Na ruksa tu niite baba watoto wako (uh, uu, uuh)
Kipingamizi hakuna juu yako (uh, uu, uuh)
Come closer nipunguze mapigo ya moyo (mapigo ya moyo)
[Chorus]
Kwa ajili yako naimba
Sauti hii sikia
Habari hii pokea
Zingatia mrembo, usipuuze mrembo
Zingatia mrembo, usipuuze mrembo
Zingatia aah aa, zingatia ahaa
[Verse 3]
Moyo wangu unatamani sana
Mimi kuwa na wewe
Acha niseme hadharani
Kila mtu asikie
Moyo wangu unatamani sana
Mimi kuwa na wewe
Acha niseme hadharani
Kila mtu asikie
Asali ni tamu baby
Kwa anayefahamu
Ila ni chungu sana
Kwa asiyefahamu
Sogea karibu yangu
Tulia kabisa
Lala kifuani kwangu
Sinzia kabisa
[Chorus]
Kwa ajili yako naimba
Sauti hii sikia
Habari hii pokea
Zingatia mrembo, usipuuze mrembo
Zingatia mrembo, usipuuze mrembo
Zingatia aah aa, zingatia ahaa

No comments:

Post a Comment